Home 2023 June 09 FARASI WA ‘TROJANI’ – SANAMU DANGANYIFU!

FARASI WA ‘TROJANI’ – SANAMU DANGANYIFU!

FARASI WA ‘TROJANI’ – SANAMU DANGANYIFU!

Moja ya hadithi maarufu ya Kiyunani ni hadithi kuhusu kutekwa kwa Jiji la ‘Troy’ moja ya mji uliokuwa maarufu katika eneo lililoitwa ‘Troad’ katika kona ya kaskazini-magharibi ya Uturuki ya sasa. Wayunani, kama unakumbuka, walilizingira Jiji hilo la Troy kwa zaidi ya miaka kumi katika Karne ya 13-12 K.K. Hawakuweza kuukamata/kuuteka mji huo. Kwa hasira, mwanamume mmoja anayeitwa Ulysses aliamua kujenga farasi mkubwa wa mbao na kumwacha nje ya kuta za Jiji hilo kama zawadi kwa Watrojani hao wasioweza kushindwa. Na kisha Wayunani wakaondoka wakisafiri kwa meli kuonyesha kushindwa kwao kwa dhahiri vita hivyo, na kumwacha farasi huyu kama zawadi; Zawadi ya hila kwa Watrojani!

“Watrojani wadadisi na wenye kiburi walijiamini vya kutosha kumburuta farasi huyo ndani ya kuta, ingawa ‘kuhani’ mmoja aliyeitwa Laucoon aliwaonya wasifanye hivyo. Laucoon alisema, ‘Ninawaogopa Wayunani, hata wanapoleta zawadi.’ Usiku huo, askari-jeshi Wayunani walijipenyeza na kutoka nje ya farasi huo, wakafungua malango ya Jiji kutoka ndani na kuruhusu vikosi vingine vya Wayunani kuingia Troy. Kisha Wayunani waliwaua watu wa Troy, wakapora mali, na kuuteketeza mji.

Daima tumezingirwa na udanganyifu na hila kama matokeo ya kazi na ushawishi wa “yule nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote” (Ufunuo 12:9). Adui yetu, Shetani, anatuletea uwongo wake kama zawadi, kama vile farasi wa Trojani. Kwa bahati mbaya, kwa miaka 2000 sasa, Kanisa, Mwili wa Kristo, limefungua milango na kuvuta mafundisho ya udanganyifu na uharibifu wa kama farasi wa Trojani. Hata hivyo, mtume wetu Paulo ametuhimiza:

“Tuyapime mambo yote; tuyashike yaliyo mema” (1 Wathesalonike 5:21)

Neno “tuyapime” linamaanisha kuchunguza, kuthibitisha au kunyambua. Hii inatupa changamoto kwa Kanisa kutokubali kudanganyika, kuwa wajinga, au kukubali kila fundisho jipya au la kuvutia linalokuja, bila ya kuchambuliwa. Tunapaswa kupima na kuchunguza mambo yote katika mwanga wa kweli isiyobadilika, isiyo na dosari ya Neno la Mungu, iliyogawanywa sawasawa. Kama Waberoya, tunapaswa kupokea neno kwa utayari wote wa akili, lakini kisha tuchunguze Maandiko kuona kama mambo hayo ndivyo yalivyo (Matendo 17:11).

Hapa kuna baadhi ya maswali mazuri ya kujiuliza wakati wa kulithibitisha fundisho: Je, fundisho hilo linamtukuza Kristo? Je, linalingana na tabia ya Mungu? Je, linategemea Maandiko? Ikiwa ndio, Je! Fundisho hilo linalingana na muktadha wa karibu wa Maandiko ambayo fundisho hilo limo? Linapatana na muktadha wa ugawaji? Linapatana na mafundisho ya Biblia kwa ujumla wake?

Baada ya kulithibitisha fundisho, maagizo ya Mtume Paulo ni kwamba “tushike sana lililo jema.” “Shika sana” maana yake ni kubaki humo, kushika umiliki thabiti. Mafundisho yanapothibitishwa kuwa mema na yanapatana na kweli ya Neno la Mungu, basi ni muhimu tuyakumbatie, tuyasimamie, na tuyaishi kulingana nayo.

Utukufu Una Yeye Kristo Milele Yote AMINA

Author: Festus Patta

4 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *