Home 2023 May 08 Kipengele cha “Wakati” Katika Maandiko!

Kipengele cha “Wakati” Katika Maandiko!

Kipengele cha “Wakati” Katika Maandiko!

Je! Ni matatizo mangapi ya Kimaandiko yangetatuliwa; Na ni mambo mangapi yanayoonekana kuwa yanapingana yangefafanuliwa; Kama tu tungekuwa waangalifu zaidi kuchunguza kipengele cha wakati, kilichokaziwa kwa nguvu sana katika Neno la Mungu?

Katika Warumi 5:12 tunajifunza kwamba dhambi iliingia ulimwenguni (kwa wanadamu wote) kupitia kwa mtu mmoja (Adamu). Kisha baadaye “sheria ikaingia” (Mstari wa 20). Lakini bado baadaye Mtume Paulo aliinuka kusema: “Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria” (Warumi 3:21).

Mapema katika historia ya mwanadamu dhabihu za damu zilihitajika ili kukubaliwa na Mungu (angalia Mwanzo 4:4; Waebrania 11:4), baadaye tohara na Sheria (Mwanzo 17:14; Kutoka 19:5), na bado baadaye; toba na ubatizo wa maji (Marko 1:4; Matendo 2:38). Lakini ni mpaka Paulo ndipo tunajifunza juu ya wokovu kwa neema kupitia imani pekee, kwa msingi wa kazi ya ukombozi iliyokamilika na ya kutosha ya Kristo.

Hii ndiyo sababu Mtume Paulo anarejelea katika Wagalatia 3:23 kwa “imani itakayofunuliwa baadaye.” Hii ndiyo sababu anatangaza kwamba Bwana wetu “alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake”, na anaongeza kusema: “ambao naliwekwa niwe mhubiri na mtume, mwalimu wa mataifa katika imani na kweli” (1 Timotheo 2:6,7).

Ni mpaka pale tu tunapotambua ‘kipengele’ cha ‘wakati’ katika Maandiko, ndipo tunapoona tofauti kati ya “ufalme wa mbinguni” na “Mwili wa Kristo,” tofauti kati ya “injili ya ufalme” na “injili ya neema ya Mungu,” tofauti kati ya “maongozi ya sheria” na “maongozi ya neema ya Mungu.”

Ulinganisho wa Warumi 3:21 na Warumi 3:26 unaonyesha jinsi kipengele hiki cha wakati kinavyosisitizwa katika Maandiko. Baada ya kujadili kazi ya Sheria katika Mistari ya 19 na 20, Mtume Paulo anatangaza: “Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria…” Kisha, katika Mstari wa 26 asema kwamba ni kusudi la Mungu: “Kutangaza, wakati huu uadilifu wake [Kristo]; ili Yeye [Mungu] awe mwenye haki na mwenye kumhesabia haki yeye amwaminiye Yesu.”

UTUKUFU NA UWEZA NA UKUU VINA YEYE HATA MILELE AMINA

Author: Festus Patta

5 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *