Home 2022 December 19 Utume Wetu Mkuu

Utume Wetu Mkuu

Utume Wetu Mkuu

Mengi yanasemwa kuhusu “AGIZO KUU” ambalo Bwana wetu Yesu Kristo aliwapa mitume wake (Thenashara) kabla tu ya kupaa kwake. Tunajiuliza iwapo wasomaji wengi wa Biblia Takatifu wamewahi kuchunguza kumbukumbu mbalimbali za utume huu kwa umakini.

Ikumbukwe kwamba “Agizo kuu hilo” halisemi neno hata moja juu ya “kuhubiriwa kwa msalaba” wala “injili ya neema ya Mungu”. “Injili” ambayo mitume wa Yesu katika mwili walitumwa kuhubiri ilikuwa ni “injili” ile ile waliyokuwa wakihubiri – Injili ya Ufalme – ambayo ndiyo wangeweza tu kuihubiri, kama ambayo Mtume Petro alivyofanya siku ya Pentekoste; kwamba Mfalme alikuwa amefufuka kutoka kwa wafu na kwamba iko siku ambayo angekalia kiti cha enzi cha Daudi.

Agizo kuu” lilihitaji imani na ubatizo kwa ajili ya ondoleo la dhambi (Marko 16:15-16); lilijumuisha uwezo wa kuponya wagonjwa na kufanya miujiza (Marko 16:17-18), lakini halikujumuisha ujumbe wa furaha kwamba “Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu” (1 Wakorintho 15:1-3). Siku ya Pentekoste, ambapo Mtume Petro alianza kutekeleza agizo hilo, aliwalaumu wasikilizaji wake kwa ajili ya kifo cha Kristo na walipotiwa hatiani kwa ajili ya dhambi yao hiyo, waliuliza: “Tufanye nini?” Mtume Petro hakusema: “Mwaminini Kristo aliyekufa kwa ajili ya dhambi zenu.” Badala yake, aliwaamuru kwa kusema “tubuni na mkabatizwe kila mmoja wenu… kwa ondoleo la dhambi” (Matendo 2:38).

Lakini baada ya Kristo na Ufalme Wake kukataliwa tena, Mungu alikatiza programu ya kinabii na kumtuma Paulo kutangaza “kuhubiriwa kwa msalaba” na “injili ya neema ya Mungu”. Katika 2 Wakorintho 5: 14-21 mtume huyu anatangaza “upendo wa Kristo” ambaye “alikufa kwa ajili ya wote” na akatuelekeza kuhusu “agizo letu kuu“:

“Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, NAYE ALITUPA HUDUMA YA UPATANISHO;

“Yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; NAYE AMETIA NDANI YETU NENO LA UPATANISHO.” (2 Wakorintho 5:18,19).

UTUKUFU UNA YEYE MILELE NA MILELE. AMINA.

Author: Festus Patta

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *