Home 2022 January 02 Kumkubali Mungu Katika Neno Lake

Kumkubali Mungu Katika Neno Lake

Kumkubali Mungu Katika Neno Lake

Kwa sababu ya kushindwa kuyaelewa makusudi ya Mungu kama yanavyoonyeshwa katika Maandiko yake, wengine wameona kuwa ‘yafaa’ kubadili mafundisho mengi yaliyo bayana katika Maandiko Matakatifu; wakifikiri kwamba Mungu hangeweza kumaanisha kile hasa Alichosema, wamehitimisha kwamba mambo haya lazima yafasiriwe katika maana ya “kiroho waliyovuviwa wao”.

Kimsingi, hakuna kitu cha kiroho katika kushindwa kumkubali Mungu katika Neno Lake, na kutafuta kufafanua ‘magumu’ kwa kubadilisha kiholela kile ambacho Mungu amekisema kwa uwazi katika Maandiko.

Kwanza, hili lingetuacha kwenye huruma ya wanatheolojia! Ikiwa Maandiko hayamaanishi yale yasemayo, ni nani aliye na mamlaka ya kuamua yale yanayomaanisha? Na tunawezaje kuligeukia Neno la Mungu ili kupata nuru ikiwa halimaanishi linachosema, na kwamba wanatheolojia waliofunzwa tu ndio wanaoweza kutuambia maana yake?

Pili, kubadilishwa huku kwa Maandiko kunaathiri ukweli wa Mungu. Lakini pia ni kuisukumia mbali heshima yake. Ikiwa maana ya dhahiri, maana ya asili ya ahadi za Agano la Kale haiwezi kutegemewa, tunawezaje kutegemea ahadi yoyote ya Mungu? Hata, Anaposema: “Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka” (Warumi 10:13), Anaweza pia akawa amemaanisha jambo lingine tofauti, badala ya lile Alilolisema hasa.

Tatu, ‘kurohozesha’ huku kwa Maandiko ni kuunga mkono uasi-imani (apostasy), kwa sababu kufanya hivyo kunawaruhusu wanadamu kubadilisha maana ya Neno la Mungu ili ‘kupatana’ na mapenzi yao.

Njia ya ufahamu wa kweli wa Biblia haiko katika ‘kuigeuza’ bali katika “kuigawanya ipasavyo” (2 Timotheo 2:15):

“Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli”

Wale ambao wamekugeukia “kurohozesha” Maandiko ya kinabii kwa sababu wameshindwa kuona kusitishwa kwa sababu ya utimilifu wake, watapata suluhisho la shida yao hiyo katika utambuzi wa utume wa kipekee na ujumbe wa Paulo.

Tambua “siri” iliyofunuliwa kupitia Mtume Paulo na hakutakuwa na haja ya kubadili unabii.

Utukufu Una Yeye Milele na Milele; Amina.

Author: Festus Patta

3 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *