Home 2024 February 05 WANAFUNZI NA MITUME

WANAFUNZI NA MITUME

WANAFUNZI NA MITUME

“Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita Mitume” (Luka 6:13).

Watu wengi wanashindwa kutofautisha kati ya wanafunzi wa Bwana wetu na mitume Wake. Wengi wanadhani wote hao wako sawa tu, kwamba wanafunzi wa Yesu ndio mitume wake. Hilo haliko sahihi, kwa kuwa Bwana wetu alikuwa na umati wa wanafunzi huku akiwa na mitume wachache. Mitume wake walichaguliwa kutoka miongoni mwa wanafunzi Wake, kama tunavyojifunza kutoka kwenye mstari uliotajwa hapo juu kutoka kwenye injili ya Luka.

Mwanafunzi ni mfuasi; mtume ni “aliyetumwa“. Mwanafunzi ni mjifunzi; mtume ni mkufunzi. Ndio kusema; Kuna somo/funzo kubwa hapa ambalo, sisi sote tunaoamini, tunatakiwa kujifunza.

Ni Lazima “tuje” kabla ya “hatujaenda”. Ni lazima tuwe “wafuasi” kabla “hatujatumwa”. Ni lazima “tujifunze” kabla “hatujafundisha”. Ni lazima “tumsikilize Bwana” kabla hatujazungumza kwa “ajili ya Bwana”.

Bwana asema hivi“, kilikuwa ni kifungu cha maneno ambacho manabii wa Agano la Kale walianzia ujumbe wao. Lakini, kwenye orodha ndefu ya manabii wa Agano hilo la Kale tunamwona nabii Samweli, akiwa kijana mdogo, akisema: “Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia” (1 Samweli 3:10).

Kabla ya kufanya au kusema chochote kwa ajili ya Mungu, basi, ni lazima tumsikilize Mungu kwanza! HII INAELEZA NI KWA NINI KUSOMA NA KUJIFUNZA NENO LA MUNGU NI MUHIMU SANA.

Kwanza, hii ndo sababu, wokovu wenyewe huja kwa kusikia na kuamini Neno la Mungu, hasa kuhusu Kristo, na kifo chake kwa ajili ya dhambi zetu. Warumi 10:17 inasema: “Imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo”, na 1 Petro 1:23 inasema: “Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele”.

Kisha, baada ya kuokolewa, sasa tunaweza kumtumikia Mungu kwa njia inayokubalika kwa kujifunza Neno Lake kwa bidii. Bila shaka, kifungu muhimu zaidi katika Biblia kuhusu jambo hili ni 2 Timotheo 2:15:

“JITAHIDI KUJIONYESHA KUWA UMEKUBALIWA NA MUNGU, MTENDA KAZI ASIYE NA SABABU YA KUTAHAYARI, UKITUMIA KWA HALALI NENO LA KWELI.”

Utukufu una Yeye KRISTO Milele na Milele AMINA

Author: Festus Patta

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *