Home 2023 April 21 “MBEROYA” NI NANI HASA?

“MBEROYA” NI NANI HASA?

“MBEROYA” NI NANI HASA?

Kuitwa Mberoya kunatokana na Matendo 17:10-11. Katika mstari wa 11 Biblia inasema kwamba watu wale wa Beroya (kwa hiyo, Waberoya) walikuwa waungwana kuliko watu wa Thesalonike kwa kuwa “walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.”

Hivyo, tunasema kwamba mtu fulani ni “Mberoya” tunamaanisha kwamba mtu huyo anafanya mambo mawili:

(1) Ana akili iliyo wazi na kupokea kwa hiari Neno la Mungu linapofundishwa kwake, na

(2) Lakini zaidi sana, baada ya hapo, anachunguza kile alichofundishwa kwa kukilinganisha na Maandiko Matakaifu. Mambo yote haya mawili, ni muhimu sana!

Baadhi ya watu wamefunga akili zao, kiasi kwamba hawataki kusikiliza kitu chochote kipya au kitu ambacho kinaweza kutishia kile wanachokijua tayari na kukiamini. Wengine ni ‘wepesi’ sana, kiasi kwamba wanakubali chochote wanachoambiwa bila kukichunguza dhidi ya yale ambayo Biblia inasema. Mambo haya yote mawili, yanapaswa kuepukwa!

Mberoya ni mtu ambaye ana maoni yenye usawaziko. Anasikiliza kile mtu anachosema kwa sababu ana shauku ya kujifunza neno la Mungu kwa ukamilifu wote. Anatambua kwamba hajajifunza na kuyafahamu yote bado. Kwa sababu hiyo, anachukua yale aliyosikia na kuyalinganisha na kile kilichosemwa katika Biblia. Kisha, kama yote mawili yanapatana, anakuwa amejifunza jambo fulani muhimu na kuongeza ujuzi wake wa Neno la Mungu, ambao umegawanywa sawasawa (2 Timotheo 2:15).

UTUKUFU UNA YEYE KRISTO YESU AMINA

Author: Festus Patta

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *