Home 2023 March 13 MUNGU “MTAKATIFU” – BIBLIA “TAKATIFU”

MUNGU “MTAKATIFU” – BIBLIA “TAKATIFU”

MUNGU “MTAKATIFU” – BIBLIA “TAKATIFU”

Tunaposema kwamba Mungu ni mtakatifu, hiyo ina maana gani kwako? Halisi? Msafi? Mkamilifu? NAAM! Lakini ufafanuzi wa utakatifu hauishii tu na uhalisia, usafi au ukamilifu. Malaika wanaokizunguka kiti cha enzi cha Mungu wanaposema kila wakati – usiku na mchana, “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu” (Isaya 6:3; Ufunuo 4:8), hawasemi tu “Halisi, Msafi, Mkamilifu,” bali wanasema zaidi ya hayo. Neno “takatifu” linamaanisha “kutengwa”. Maandiko yanapotangaza kwamba Mungu wetu, ndiye mtakatifu (Zaburi 99:9), yana maana kwamba Yeye si kama mwingine yeyote yule. Hakuna kama Yeye; Yeye hana kifani na hawezi kulinganishwa; Hakuna aliye sawa naye; Yeye ni wa kipekee ndani Yake na Nafsi Yake; Asiye na kifani katika uzuri, thamani, na ukamilifu. Ametengwa kwa ajili Yake; Kama inavyosemwa, “Mungu daima ni kitu kikubwa zaidi katika kuwepo.”

Biblia inaporejelewa kuwa ni “Maandiko matakatifu” (2 Timotheo 3:15), “matakatifu” yanamaanisha kitu kile kile. Biblia si kama kitu kingine chochote kile. Hakuna kitabu kingine kama hicho; Haina usawa; Hailinganishwi; Haina kifani katika uzuri wake, thamani, na ukamilifu wake. Biblia imetengwa na vitabu vingine vyote; NI NENO LA MUNGU!

UTUKUFU UNA YEYE MUNGU MILELE NA MILELE AMINA

Author: Festus Patta

One Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *