Home 2023 February 21 KUTAZAMIA “UFUFUO” ULIO BORA ZAIDI!

KUTAZAMIA “UFUFUO” ULIO BORA ZAIDI!

KUTAZAMIA “UFUFUO” ULIO BORA ZAIDI!

Wakati umati wa Wababiloni uliposujudu kuabudu mbele ya mungu wa dhahabu ambaye Nebukadreza alikuwa amesimamisha, Waebrania watatu walikataa ‘kuinama’ na wakabaki ‘wamesimama’, wima na peke yao.

Walipoitwa mbele ya Nebukadreza kujibu kwa nini hawakuinama mbele ya mungu wa kuchongwa na kutishiwa kifo katika tanuru ya moto, walijibu:

“Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme. Bali kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha” (Danieli 3:17- 18).

Huu ndio msimamo ambao kila muumini anapaswa kuuchukua kwa ajili ya Mungu na kweli yake. Ana uwezo wa kutukomboa kutoka kwenye mateso ikiwa tunasimamia kweli yake, lakini hata kama Yeye haoni inafaa kufanya hivyo bado tunapaswa kusimama peke yetu, ikiwa ni lazima, kwa ile nuru aliyotupatia kutoka kwenye Neno lake.

Wengi wamepata hasara kwa kitambo kwa ajili ya kutetea imani zao. Waebrania 11 inaorodhesha miongoni mwa baadhi mashujaa wa imani ambao “waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora,” na wengine ambao “walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani; walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya” (Wabrania 11:35-37).

Lakini tunasoma kwamba hawa wote “walipata habari njema” mbele za Mungu na kutazamia “ufufuo ulio bora zaidi” (Mistari ya 35, 39).

Uasi unapoongezeka sana, hasa miongoni mwa ‘watumishi’; Wale wanaosimama katika kweli ya Neno la Mungu, mara nyingi hudhihakiwa na kudharauliwa! Mungu atupe neema ya kusimama katika kweli Yake, bila kujali gharama, tukikumbuka kwamba mateso yoyote kwa ajili ya Kristo ni ya muda tu wakati thawabu zitakuwa ni za milele.

UTUKUFU UNA YEYE MILELE NA MILELE AMINA

Author: Festus Patta

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *