Home 2022 July 08 WABEROYA!

WABEROYA!

WABEROYA!

“Mberoya” ni nani?

Kuitwa Mberoya, kunatokana na Matendo 17:10-11:

“Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi. Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.”

Katika mstari wa 11 Biblia inasema kwamba wale watu wa Beroya (kwa hiyo, Waberoya) walikuwa ni waungwana kuliko wale wa Thesalonike kwa sababu “walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo”, na “wakayachunguza maandiko kila siku”, ili waweze kuona kama “mambo hayo ndivyo yalivyo.”

Hivyo, tunaposema kwamba mtu fulani ni “Mberoya” tunamaanisha kwamba mtu huyo ana sifa kuu mawili:

(1) Ana akili iliyo wazi na kupokea kwa hiari Neno la Mungu linapofundishwa kwake, na

(2) Lakini baadae, anakichunguza kile alichofundishwa kwa kukilinganisha na Maandiko.

Mambo yote hayo mawili ni muhimu sana!

Kuna baadhi ya watu wamefunga kabisa ‘fahamu’ zao kiasi kwamba hawataki kusikiliza chochote kipya au kitu ambacho kinaweza ‘kutishia’ kile wanachokijua tayari. Wengine ni ‘wajinga’ zaidi kiasi kwamba wanakubali chochote wanachoambiwa bila ya kukichunguza dhidi ya yale ambayo Biblia inasema. ‘Kupindukia’ kote huko kuwili kunapaswa kuepukwa…

Mberoya ni mtu ambaye ana maoni yenye usawaziko. Tunasikiliza kile mtu anachosema kwa sababu tuna shauku ya kujifunza neno la Mungu kwa ukamilifu zaidi; Kwa sababu tunatambua kwamba bado hatujajifunza na kuyajua yote.

Hivyo, tunayachukua yale yote tuliyosikia na kuyalinganisha na Biblia. Ndio kusema, ikiwa mambo hayo yanapatana, tunakuwa tumejifunza jambo fulani jipya na kuongeza ujuzi wetu katika Neno la Mungu, ambao umegawanywa sawasawa.

Utukufu una Yeye KRISTO, Milele na Milele; AMINA.

Author: Festus Patta

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *