Home 2022 July 07 Roho ya Imani

Roho ya Imani

Roho ya Imani

Ni jambo la ‘kusisimua’ kumsikia Mtunga Zaburi, ingawa “alikuwa katika mateso”, akisema: “Naliamini, kwa hiyo nalisema” (Zaburi 116:10)!

Inasisimua zaidi, kumwona Mtume Paulo, ingawa alikuwa katika “kiudhiwa…, kutaabishwa…, kufadhaishwa…, kuteswa…, kutupwa chini…, kutolewa ili afe kwa ajili ya Yesu” – lakini pamoja na yote hayo, ni jambo la kutia moyo kumuona Paulo naye akichukua msimamo; kama wa Daudi na tunamsikia akiitamka “ROHO ILE ILE YA IMANI”, na kuongeza kusema:

“TWAAMINI NA KWA SABABU HIYO TWANENA” (2 Wakorintho 4:8-13)

Laiti kama wale wote wanaoamini ujumbe mtukufu wa neema ya Mungu: Kwamba waaminio katika Kristo wamekubaliwa ndani Yake, na kutamkwa kuwa wako “kamili” na wamebatizwa katika mwili mmoja kwa ubatizo mmoja wa kiungu – kama wote hao, wanaoamini kweli hizi, WANGENENA leo kungekuwa na ufufuo mkubwa kesho katika Kanisa, Mwili wa Kristo…

Iwapo, wangeweza kuweka pembeni ‘mazingatio’ mengine yote, na kusema kwa uwazi na kwa uaminifu: “TWAAMINI NA KWA SABABU HIYO TWANENA”, matokeo yake yangekuwa ni ushindi mkubwa kwa Kanisa na yenye kutufikisha mbali kuliko hapa ‘tulipokwamia’ sasa! Hata hivyo, pamoja na yote hayo, bado wanapaswa KUSEMA, kwa maana hii ni “roho ya imani“.

Lakini, katikati ya hayo, wapo wachache walio na “roho ya imani”; wachache ambao wamesimama, bila kujali matokeo, kwa sababu ya ile nuru ambayo Mungu amewaangazia. Wapo wengine ambao wameamua ‘kudumisha busara’ ya ukimya kwa sababu ya “hofu ya wanadamu”; wengine wanafanya hivyo kwa sababu wanapenda “sifa za mwanadamu”. Makundi yote hayo mawili yanasema: “Mtu ni lazima awe mwangalifu na kile anachokisema, kwa sababu kweli hizi sio maarufu”; ingawa wote hao, mioyoni mwao, wamejawa na hatia ya kutokuwa waaminifu kwa MUNGU na kwa KWELI.

Kwa msaada wa Mungu, kamwe tusiwe miongoni mwa makundi hayo. Sisi lakini, pale kweli inapohusika, tusimame pamoja na Daudi na Paulo na kusema: “TWAAMINI NA KWA SABABU HIYO TWANENA!” Na hivyo tuwe miongoni mwa wale walio na “roho ya imani”, na walioazimia “kusimama imara na hodari katika imani” na kuwa tayari “kupigana vita vile vizuri vya imani” (1 Wakorintho 16:13; 1 Timotheo 6:12).

Utukufu una Yeye KRISTO, Milele na Milele; AMINA.

Author: Festus Patta

One Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *