Home 2022 May 13 “KWELI” NI NINI…???

“KWELI” NI NINI…???

“KWELI” NI NINI…???

Biblia ni ya kipekee miongoni mwa vitabu vyote kama vile alivyo Kristo miongoni mwa wanadamu, kwa kuwa ndicho kitabu pekee kinachodai mara kwa mara na kwa mfululizo kuwa ni KWELI.

Biblia inaanza na maneno haya yenye fahari:

“Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.”

Haijadiliani wala Haishindani; inaeleza tu kwa urahisi KWELI hiyo!

Utangulizi wa kidhabihu kwa nabii ni huu: “Bwana asema hivi,” na nabii mia kadhaa zilizotimizwa, zinathibitisha kwamba Biblia kwa HAKIKA ni Neno la Mungu – ni KWELI.

Bila kuhitaji maoni ya mwanazuoni, Biblia inarejelea:

“Udhihirisho wa KWELI” (2 Wakorintho 4:2).

“Ujuzi wa KWELI” (2 Timotheo 3:7).

Wale “walioikosa ile KWELI” (2 Timotheo 2:18).

Wale “wanaopingana na ile KWELI” (2 Timotheo 3:8).

Wale “waipingao KWELI kwa uovu” (Warumi 1:18).

Wale “wanaogeuza masikio yao wasisikie yaliyo KWELI” (2 Timotheo 4:4).

Wale “walio na imani wenye kuijua hiyo KWELI” (1 Timotheo 4:3).

Wale “wenye ujuzi wa KWELI ile iletayo utauwa” (Tito 1:1).

Bwana wetu alimwambia Baba yake: “Neno lako ndiyo kweli” (Yohana 17:17).

Paulo aliwaandikia wale wote waliookolewa kwa “kulisikia neno la KWELI, habari njema za wokovu wao” (Waefeso 1:13).

Pale ambapo KWELI inahusika, Neno la Mungu ndilo PEKEE tunalohitaji, kwa sababu:

“Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

“Ili mtu wa Mungu awe kamili, AMEKAMILISHWA apate kutenda kila tendo jema.” (2 Timotheo 3:16,17).

Na KWELI sio sawa na “ukweli”!!!

Author: Festus Patta

One Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *