Home 2022 April 16 Kifo cha Kristo Kwa Ajili Yetu

Kifo cha Kristo Kwa Ajili Yetu

Kifo cha Kristo Kwa Ajili Yetu

Mara tatu katika Sura ya 5 ya waraka wa Paulo kwa Warumi, tunasoma kwamba, “Kristo alikufa kwa ajili yetu”!

Mstari wa 6: “Kwa maana hapo tulipokuwa hatuna nguvu, wakati ulipotimia, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu.”

Mstari wa 8: “Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi.”

Mstari wa 10: Kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake; zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake.”

Hivyo, katika unyonge wetu; katika hali yetu ya dhambi; hata katika utashi wetu, Kristo alitupenda na kutoa uhai yake ili kutuokoa. Lakini ni kwa nini Mtume Paulo anasema kwamba Kristo alikufa kwa ajili yetu:

  • “Tulipokuwa bado hatuna nguvu,”
  • “Tulipokuwa bado wenye dhambi” na
  • “Tulipokuwa adui”?

Je! Si kweli kwamba, Kristo hakufa kwa ajili yetu kabla hata mmoja wetu hajazaliwa?

Ni kweli, hivyo ndivyo ilivyo; lakini hapa Mtume Paulo anaandika kihistoria kuihusu jamii yote ya wanadamu. Sehemu iliyobaki ya Sura hiyo ya 5, inathibitisha hilo!

Katika Mstari wa 12 anamrejelea Adamu, “mtu mmoja” ambaye kupitia kwake dhambi na kifo viliingia ulimwenguni. Huyu ndiye alimfanya kila mmoja wetu kuwa hoi kweli kweli na ‘furushi’ la dhambi. Katika Mstari wa 20 anamrejelea Musa, ambaye “sheria iliingia kupitia yeye, ili kosa lile lizidi kuongezeka.” Hivyo kwa sheria watu wote walihukumiwa kuwa wenye dhambi. Hatimaye, katika Mistari ya 20, 21, anamrejelea Kristo, “aliyekufa kwa ajili ya wote” (2 Wakorintho 5:14-15), ili kwamba wenye dhambi ‘wasiojiweza’ wapate kuokolewa; Naam, hata adui za Mungu wapate kupatanishwa Naye kwa neema, kwa njia ya imani. Kwa Adamu tuna mlango wa dhambi, kwa Musa tuna hukumu ya dhambi na kwa Kristo tuna msamaha wa dhambi…

Hatua kwa hatua, umuhimu wa kifo cha Kristo kwa wanadamu wote ulifunuliwa, lakini sasa tunajua kwamba watakatifu wa nyakati zote wameokolewa kwa msingi wa kifo cha Bwana wetu pekee. Hakuna mtu mwingine hata mmoja ambaye angeweza kulipa deni kubwa hivyo la dhambi.

Hivyo, katika hali yetu ya unyonge, katika hali yetu ya dhambi, naam, tumshukuru Mungu, katika uadui wetu, Bwana wetu Yesu Kristo alikufa ili atuokoe.

“MWAMINI BWANA YESU, NAWE UTAOKOKA” (MATENDO 16:31)

Author: Festus Patta

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *