Home 2021 October 30 Baraka ya Kweli

Baraka ya Kweli

Baraka ya Kweli

Ni jambo lisilojulikana na wengi kwamba neno “kubarikiwa,” katika Biblia zetu, linamaanisha tu kuwa na ‘furaha’. Hivyo “mtu mwenye heri” wa Zaburi 1:1 [(Heri = blessed(Kiingereza) = ‘esher(Kiebrania)] ni mtu mwenye furaha na “Mungu ahimidiwaye” wa kwenye 1 Timotheo 1:11 [(Ahimidiwaye = blessed(Kiingereza) = makarios(Kigiriki)] ni Mungu mwenye ‘furaha’. (Tumeyarejelea maneno ya Kiebrania na Kigiriki ambayo mara nyingi hutafsiriwa ‘kubarikiwa’).

Kwa maneno machache, kutokujulikana huko kunatokana na kuwa na ufahamu wa juujuu, au kukosa uelewa wa moja ya maneno muhimu zaidi ya Maandiko. Mpumbavu anaweza kuwa na ‘furaha’, mlevi anaweza kuwa na ‘furaha’, mtu mwovu anaweza kuwa na ‘furaha’, lakini hakuna hata mmoja kati ya hao ambaye kiukweli amebarikiwa, kwa sababu mtu aliyebarikiwa anayo sababu nzuri/kubwa zaidi ya ‘kushangilia’.

Hiyo ndiyo sababu Zaburi 1:1-2 inasema kwamba mtu ambaye huepuka “shauri la wasio haki”, “njia ya wakosaji” na “baraza la wenye mizaha” na kutafakari na kufurahia sheria ya Mungu, “amebarikiwa” – ANA HERI!  Yeye ni ‘tajiri’ (ana hali nzuri) na anayo sababu kubwa zaidi ya kufurahi.

Ni wachache, bila shaka, wangethubutu kudai kwamba wameishi kikamilifu kulingana na kifungu hicho cha Zaburi. Neno la Mungu, hata hivyo, lina habari njema kwa ajili ya hao. Katika Warumi 4:6-8, Mtume Paulo anatuambia maneno haya:

“Kama vile Daudi aunenavyo uheri wake mtu yule ambaye Mungu amhesabia kuwa na haki pasipo matendo, Heri waliosamehewa makosa yao, Na waliositiriwa dhambi zao. Heri mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi”

Baraka (Heri) hii sio hisia tu ya kuwa na furaha. Badala yake, ni hali halisi ya kuwa na ‘hali-njema’; huku ukiwa na sababu ya kina na inayokudumisha katika kuwa na furaha hiyo ya kweli.

Kwa hiyo Zaburi 40:4a inasema: “Heri aliyemfanya Bwana kuwa tumaini lake,” na Wagalatia walipoacha kumtumainia kabisa Bwana na kuanza kuyategemea matendo yao wenyewe, Mtume Paulo aliwauliza: “Ku wapi, basi, kule kujiita heri?” (Wagalatia 4:15a).

Hivyo basi, ‘kubarikiwa’ kiuhalisia ni kuwa na ‘hali-njema’; na kuwa na sababu kubwa zaidi ya kufurahi. Hii ndiyo sababu mwamini katika Kristo, aliyeokolewa na mwenye salama ya milele ndani Yake, ni kama Mungu Mwenyewe alivyo, “amebarikiwe milele.”

Utukufu na Ukuu na Uweza na Nguvu Vina Yeye Milele na Milele, AMINA

Author: Festus Patta

3 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *