Ushindi wa Imani
“Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu” (1 Yohana 5:4)
Kuna watu wengi wanaoitazama imani kama kitu cha kufikirika. Wengine wanadhani imani ni kuangalia tu upande mmoja ‘angavu’ wa mambo; kwa wengine ni utashi; na bado wapo wengine wanaochanganya imani na mitazamo yao binafsi.
Katika Biblia, imani ni kumwamini Mungu tu. “Imani” ni nomino na “kuamini” ni kitenzi. Hili linaonekana katika Warumi 4:5, ambapo Mtume Paulo anaeleza haya:
“Lakini kwa mtu asiyefanya kazi, bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtauwa, imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki”
Kifungu tulichoanza nacho hapo juu kutoka 1 Yohana 5 pia kinaweka wazi jambo hili, kinapoangaliwa katika muktadha wake:
“Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu. Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu?” (Mstari wa 4-5)
Ndio kusema, mwamini katika Kristo; na ni mwamini katika Kristo pekee, ndiye awezaye kuushinda ulimwengu. Wote wasioamini ‘wanafagiliwa’ mbali kwa majigambo yao juu ya mfumo wao wa ulimwengu huu!
Mtume Paulo, kwa uongozi wa Roho Mtakatifu, alisema kwamba wasioamini wanaifuata “kawaida ya ulimwengu huu,” inayoongozwa na shetani, “roho atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi” (Waefeso 2:2):
“Ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi”
Hatuna maana kusema kwamba wanaoamini hawashawishiwi mara kwa mara kufuata “kawaida ya ulimwengu huu.” Kimsingi, kuna wakati fulani ulimwengu unatushawishi na kututisha, lakini “HUKU NDIKO KUSHINDA KUUSHINDAKO ULIMWENGU, HIYO IMANI YETU.”
Kwa Utukufu Wake Kristo Yesu
Leave a Reply