Home 2021 September 15 Yote ‘KWA AJILI YETU’

Yote ‘KWA AJILI YETU’

Yote ‘KWA AJILI YETU’

Je! Umewahi kufikiria ni kwa kiasi gani Mungu wetu amefanya yote “KWA AJILI KWETU” katika Kristo Yesu?

Katika Warumi 8:32 tunasoma kwamba Mungu katuokoa kutoka dhambini, na ya kwmba “hakumwachilia Mwanawe, bali alimtoa KWA AJILI YETU sisi sote”…

“Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?”

Katika Tito 2:14 tunaambiwa kwamba Kristo “alijitoa mwenyewe KWA AJILI YETU, ili atukomboe kutoka katika uovu wote”…

“Ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema”

Katika Warumi 5:8 Mtume Paulo anatutangazia kwamba “tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa KWA AJILI YETU”…

“Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi”

Nayo Wagalatia 3:13 inasema kwamba Kristo “alifanywa laana KWA AJILI YETU”…

“Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti”

Waefeso 5:2 inasema kwamba Kristo “alifanyika kuwa dhabihu kwa Mungu KWA AJILI YETU”…

“Mkaenende katika upendo, kama Kristo naye alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato”

Waebrania 9:12 inasema kwamba “Aliingia… katika patakatifu [pale Baba alipo], akiisha kupata ukombozi wa milele KWA AJILI KWETU”. Na ikiwa tunamwamini Yeye kwa ajili ya “ukombozi huu wa milele” tunaweza kusoma zaidi katika Waebrania 9:24 kwamba “Kristo hakuingia katika patakatifu palipofanyika kwa mikono…; bali aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu KWA AJILI YETU”.

Warumi 8:34 inahoji ni nani awezaye kumhukumia adhabu mwamini wa Kristo, kwa sababu YEYE [Bwana Yesu Kristo] sasa yuko “mkono wa kuume wa Mungu” na ndiye “anayetuombea“?

Waebrania 6:20 inasema kwamba Bwana wetu aliingia ndani ya pazia, mbele ya Baba, “KWA AJILI YETU” kama “Mtangulizi” wetu. Zaidi ya hayo, Waebrania 10:19-20 inawahimiza waamini kuwa na ujasiri wa kupaingia patakatifu pa Mungu kwa maombi:

“Basi, ndugu, tukiwa na ujasiri wa KUINGIA katika patakatifu kwa damu ya Yesu… njia mpya na hai, ambayo ameitakasa KWA AJILI YETU”

Hebu kuwa muugwana; Fikiria ni mengi kiasi gani Mungu ametufanyia sisi katika Kristo Yesu? Alimtoa Mwanawe mpendwa KWA AJILI YETU, Kristo alijitoa mwenyewe KWA AJILI YETU, alikufa KWA AJILI YETU, akawa laana KWA AJILI YETU, anatuombea, akaingia mbinguni kama Mtangulizi WETU, na kuweka wakfu “njia mpya na iliyo hai” ya kuelekea mbele za Mungu KWA AJILI YETU, ili tuweze “kukikaribia kwa ujasiri kiti cha neema” ili “tupewe rehema, na kupata neema ya kusaidia wakati wa mahitaji” (Waebrania 4:16).

BASI, TUSEME NINI JUU YA HAYO? MUNGU AKIWAPO UPANDE WETU, NI NANI ALIYE JUU YETU? (WARUMI 8:31)?

Author: Festus Patta

7 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *