Home 2021 May 16 Fundisho Ni Nini?

Fundisho Ni Nini?

Fundisho Ni Nini?

Biblia inaeleza kuhusu mafundisho kuwa ni maagizo, maarifa, au maudhui yaliyomo kwenye kile kinachofundishwa. Katika Mithali tunasoma maneno haya:

“Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu, Tegeni masikio mpate kujua ufahamu. Kwa kuwa nawapa mafundisho mazuri; Msiiache sheria yangu” (Methali 4:1-2)

Na katika Isaya, imeandikwa:

“Atamfundisha nani maarifa? Atamfahamisha nani habari hii?…” (Isaya 28:9a)

Biblia inaonya kwamba kuna mafundisho mengi ulimwenguni na inaweza kuwa rahisi kwa Mkristo asiye na msimamo, asiye imara kuchukuliwa na mafundisho hayo yasiyo ya kweli. Katika Waefeso, Paulo anatuhimiza tuwe imara katika Neno la Mungu:

“Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu” (Waefeso 4:14)

Badala yake, tunapaswa “kujifunza kujionyesha kuwa tumekubaliwa na Mungu” tukijifunza mafundisho ya Mungu yanayopatikana katika Biblia. Paulo anamwagiza Timotheo kwa kumwambia hivi:

“Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha” (1 Timotheo 4:13)

“Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki” (2 Timotheo 3:16)

Zaidi ya hayo, haitoshi tu kuwa na mafundisho, bali ni lazima tuwe na mafundisho yenye uzima ambayo yanatuhusu sisi katika kipindi hiki cha majira ya neema ya Mungu. Mafundisho aliyopewa Nuhu ya kujenga safina katika Mwanzo 6 yatakuwa mafundisho yasiyo na uzima kwangu mimi na kwako wewe kufuata leo:

“Lakini wewe nena mambo yapasayo mafundisho yenye uzima” (Tito 2:1)

Vivyo hivyo ‘mafundisho mazuri’ ya sheria katika Mithali 4:2 yangekuwa pia ni mafundisho yasiyofaa kwetu leo ​​katika kipindi hiki cha Neema, ingawa yalikuwa ‘mafundisho mazuri’ katika kipindi kile cha Sheria.

Leo, ni lazima tujihadhari na wale ambao wanaweza kutudanganya na mafundisho yao yasiyo na msingi ambayo yanaweza kuturudisha nyuma na kutuweka tena chini ya kifungo cha sheria.

Mtume Paulo amemhimiza sana Timotheo kuwa makini na walimu hawa wa sheria, pale alipomwagiza:

“… Uwakataze wengine wasifundishe elimu nyingine” (1 Timotheo 1:3b)

Kwa kuwa alikabidhiwa uwakili wa Neema ya Mungu (Waefeso 3:1-2), Mtume Paulo anatuagiza, kwa kusema maneno hayo juu ya mtumishi wa Mungu kwamba anatakiwa awe:

“akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga” (Tito 1:9)

Kwa Utukufu wa Jina la Kristo Yesu

Author: Festus Patta

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *