Home 2020 March 02 Karama ya Kufundisha

Karama ya Kufundisha

Karama ya Kufundisha

Je, karama ya ualimu huonekana kama nini?

Je, ni miaka mingi ya kujifunza kwa maneno na matendo, imla, na muktadha?

Je, inaonekanaje kuwa ni zawadi wakati mtu anatakiwa aifanyie kazi, ajifunze?

Vipi kuhusu masaa ya maandalizi, uhariri, na mazoezi?

Kutokana na hayo, haionekani kama kuwa ni zawadi, bali hiyo ni kazi, tena ngumu!

Je, ni wakati watu wanapenda kusimama mbele ya wengine na kutoa maoni yao?

Kama hiyo ni kweli, basi kila mwenye ‘blog’ ana karama ya Mungu ya kufundisha!!!

Ukweli ni Mungu hatoi karama ya kimungu ya kufundisha tena. Ametuthifadhia Kitabu cha kujifunza kutoka kwacho; kinaitwa BIBLIA!

Uwezo wa kufundisha huja kutoka kwa watu waaminifu wanaowafundisha wengine jinsi ya kuelewa neno la Mungu:

“Na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine” (2 Timotheo 2:2)

Kuna walimu wengi sana wabaya ambao wanadai kuwa wana kipawa cha kufundisha. Wale wabaya zaidi hutumia ‘kisingizio’ hicho (kwamba wana karama) kama mbadala wa kutojifunza fundisho la Kristo.

Huna haja ya kipawa kutoka kwa Mungu ili kufundisha. Unahitaji ‘hamu’ na kutumia muda wako kujifunza nyenzo za kufundishia.

Tunahitaji walimu zaidi, na sio karama zaidi (2 Timotheo 2:15)

Kwa Utukufu wa Jina Lake…; AMINA.

Author: Festus Patta

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *