Home 2024 June 09 HATA KAMA MUNGU “AKINYAMAZA”!

HATA KAMA MUNGU “AKINYAMAZA”!

HATA KAMA MUNGU “AKINYAMAZA”!

Wakati uma wa Wababiloni uliposujudu kuabudu mbele ya mungu wa dhahabu ambaye Nebukadneza alikuwa amemsimamisha, Waebrania watatu walikataa kusujudu na kubaki wamesimama, wima, peke yao.

Walipoitwa mbele ya Nebukadneza kujibu mashitaka kwa sababu ya kukataa kwao kusujudu na hata baada ya kutishiwa kifo katika tanuru ya moto, wao walijibu kwa kusema hivi:

“Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme. Lakini kama sivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha” (Danieli 3:17-18).

Huu ndio msimamo ambao kila muumini anapaswa kuuchukua kwa ajili ya Mungu na kweli yake; Naye anaweza kutukomboa kutoka kwenye mateso kama tu tunasimamia ukweli, na hata kama Yeye haoni vyema kufanya hivyo, bado tunapaswa kusimama peke yetu ikiwa ni lazima, kwa sababu ya ile nuru ambayo ametupa kwenye Neno Lake.

Watu wengi wamepata mateso ‘kwa muda’ kwa sababu ya kusimama kikamilifu katika imani zao.  Waebrania 11 inaorodhesha miongoni mwa mashujaa wa imani, baadhi ya watu ambao “waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora; wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani; walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya” (Waebrania 11:35-37).

Lakini tunasoma kwamba hawa wote “walipata sifa njema” mbele za Mungu na kuutazamia “ufufuo ulio bora zaidi” (mistari ya 35,39).

Uasi unapoongezeka katikati yetu na wale wanaosimama katika ukweli ya Mungu, mara nyingi hudhihakiwa na kudharauliwa; Mungu atupe neema ya kusimama katika kweli bila kujali gharama, huku tukikumbuka kwamba mateso yoyote yale juu ya Kristo ni ya kitambo tu, wakati thawabu za kusimama katika kweli ya Mungu ni za milele.

Utukufu una Yeye KRISTO YESU Milele na Milele AMINA

Author: Festus Patta

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *