Home 2021 June 15 Mungu “Mtakatifu” – “Biblia Takatifu”

Mungu “Mtakatifu” – “Biblia Takatifu”

Mungu “Mtakatifu” – “Biblia Takatifu”

Tunaposema kuwa Mungu ni mtakatifu, hiyo huwa inamaanisha nini kwako? Kwamba Mungu ni Msafi? Ndio; Mungu ni Msafi! Lakini maana halisi ya utakatifu haiishii tu kwenye usafi…

Wakati malaika wanapozunguka kiti cha enzi cha Mungu, bila kupumzikia wakati wote wakisema, “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu” (Isaya 6:3; Ufunuo 4:8), hawasemi tu “Msafi, Msafi, Msafi,” bali wanasema zaidi ya hayo. Neno “takatifu” linamaanisha kutengwa…

Wakati Maandiko yanapotangaza kwamba Mungu ni mtakatifu (Zaburi 99:9), yanamaanisha kwamba Yeye si kama mwingine yeyote yule. Hakuna aliye kama Yeye. Halingani na wala halinganishwi. Hakuna aliye sawa naye. Yeye ni wa kipekee ndani yake na Nafsi Yake, asiye na kifani katika uzuri, thamani, na ukamilifu. Amejitenga mwenyewe kwa ajili yake. Kama inavyosemwa, “Mungu ndiye kitu kikuu, kupita vyote katika maisha”…

Pale ambapo Biblia inarejewa kama “Maandiko matakatifu” (2 Timotheo 3:15), “takatifu” inamaanisha jambo lile lile. Biblia haifanani na kitu kingine chochote. Hakuna kitabu kingine kama hicho. Haina usawa. Hailinganishwi, haina kifani katika uzuri wake, thamani yake, na ukamilifu. Biblia imetengwa na vitabu vingine vyote. Ni Neno la Mungu…

Kwa Utukufu Wake Kristo

Author: Festus Patta

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *