Je, Nini Maana ya Biblia Kuwa ni Pumzi ya Mungu?
Wakati watu wanasema kuwa Bibilia ni pumzi ya Mungu, huwa wanarejelea dhana kuwa Mungu kwa uungu wake alishawishi uandishi wa Bibilia kwa mwanadamu kwa njia ambayo chochote walichokiandika ni neno la Mungu. Kwa mujibu wa Bibilia, neno ‘pumzi’ linamaanisha ‘Mungu aliwafanyia imla au aliwafunulia’. Pumzi inamaanisha kwamba Bibilia kweli ni neno la Mungu na inafanya Bibilia kuwa ya ajabu kati ya vitabu vyote.
Ingawa kuna mabishano kuwa ni kwa kiwango gani Bibilia ni pumzi ya Mungu, bila ya tashwishi yoyote, Bibilia yenyewe inasema kuwa kila neno katika Bibilia linatoka kwa Mungu (1 Wakorintho 2:12-13; 2 Timotheo 3:16-17). Pumzi hii imeenea katika sehemu zote za Bibilia na katika kila malengo makuu ya Bibilia. “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila kazi njema” Hii aya inatuambia kwamba Mungu aliweke pumzi yake kwenye Bibilia yote na ni kwa ajili ya manufaa yetu. Maana yake ni kwamba sio tu katika sehemu za Bibilia ambazo zinashughulika na imani tu ndizo zina pumzi ya Mungu, bali ni kila neno lililopo kwenye Biblia, kuanzia Mwanzo hadi Ufunuo, lina pumzi ya Mungu.
Kwa sababu hiyo, Bibilia ina mamlaka yote katika imani, na yatosha kwa mafundisho na maonyo kwa kila binadamu kwa jinsi ambavyo anatakiwa kuwa na uhusiano mema na Mungu. Bibilia haisema tu ina pumzi ya Mungu pekee, bali pia ina uwezo wa kutubadilisha na kutufanya tuwe ‘wakamilifu’ Je, tunaihitaji nini zaidi? Sura nyingine inayozungumzia kuwa Bibilia ina pumzi ya Mungu ni 2 Petero 1:21. Sura hii inazidi kutueleza kuwa hata kama Mungu alitumia wanadamu kwa maumbile yao tofauti, na namna ya uandishi wao, Mungu kwa uungu wake, aliwafunulia lile neno waliloliandika. “Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu” Yesu mweneywe alithibitisha pumzi ya Mungu kwenye Bibilia pale aliposema, “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka, hata yote yatimie” (Mathayo 5:17-18).
Katika misitari hii, Yesu anatilia mkazo juu ya ule ukamilifu wa maandiko ya Bibilia na kwamba hata lile elezo dogo, kama nukta, halitaondoka kwa sababu ni neno la Mungu. Kwa sababu Bibilia ina pumzi ya Mungu, tunaweza kumalizia kusema kwamba ni kamilifu, na kwa sababu hiyo ina mamlaka yote. Na kwa sababu pia Mungu ni mwenye uwezo wote, anayejua mambo yote, na ni mkamilifu, neno lake pia litakuwa na taswira yake na kuwa na tabia zile zile kama zake.
Leave a Reply