Home 2024 September 03 MAADUI WA MUNGU NA WAABUDU WA SHETANI

MAADUI WA MUNGU NA WAABUDU WA SHETANI

MAADUI WA MUNGU NA WAABUDU WA SHETANI

“Kwa maana ikiwa TULIPOKUWA ADUI tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake; zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake” (Warumi 5:10)

“Ambao ndani yao MUNGU WA DUNIA HII AMEPOFUSHA FIKIRA ZAO WASIOAMINI, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu” (2 Wakorintho 4:4)

Watu wengi wa kidini, hususani wale ambao hawajaokoka, hawatakubali ukweli kwamba wao ni maadui wa Mungu, na kushindwa kuelewa kwa nini Biblia inaendelea kusisitiza kwamba wao ni wenye dhambi. Lakini Mungu, yule anayesema kwamba wao ni wenye dhambi, na kwamba ni wenye kustahili hukumu ya milele; Ndiye anayesema kwamba, tumaini lao pekee la wokovu liko kwa Yule aliyemwaga damu ya uhai Wake, pale Kalvari, ili kulipa adhabu ya dhambi zao – Mungu huyu, Mungu wa Biblia, wao hawawezi kumuishi!

Itokee mmoja wa watumishi Wake mwaminifu, awaambie ndugu hao, yale Mungu huyo wa Biblia anayoyasema juu yao – atatukanwa! Mungu huyu, Mungu wa kweli, Mungu wa Biblia, anapokataa kuzikubali kazi zao “nzuri” au mwenendo wao “wa haki”; ndugu hawa hutenda kama Kaini, ambaye tunasoma haya kumhusu katika Mwanzo 4:5: “Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana”. Watu hawa, hawatamsujudia Mungu huyu wa Biblia, na mtazamo wao huo ni usaliti na ni uadui wao dhidi Yake.

Lakini je, ni kwa nini watu hawa hawatageuka kutoka katika kujihesabia haki na kumwamini Kristo, ambaye alikufa kwa ajili ya dhambi zao? Ni kwa sababu tu, ndugu hao, wanamwabudu Shetani, “mungu wa nyakati hizi,” ambaye “amepofusha fikira zao wasioamini.” Kwamba, watu hawa, wanamwabudu Shetani? Hili pia, ni jambo ngumu kwa mtu ambaye hajazaliwa upya kuliamini juu yake yeye mwenyewe. Kama vile alivyo na dhana yake yeye mwenyewe juu ya Mungu, na ndivyo alivyo na dhana yake mwenyewe juu ya Shetani – iliyokosewa!

Watu wasioamini, hawajui kwamba, Shetani anayenenwa kwenye Biblia ni halisi, naye kwamba ana ‘kabati kubwa la nguo’ na katika kipindi hiki cha neema, bila shaka, anaonekana mara nyingi zaidi kama “malaika wa nuru” pamoja na “wahudumu wa haki” (2 Wakorintho 11:14-15). Hakika, huyu Shetani, ndiye wanayemuabudu, na kumheshimu, na kujaribu kuishi kwa kanuni zake, wakiamini kwamba, njia ya wokovu ni kufanya kwa viwango vyao…

Utukufu una Yeye KRISTO YESU Milele na Milele AMINA

Author: Festus Patta

2 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *