Home 2024 August 17 MWANA WA ADAMU!

MWANA WA ADAMU!

MWANA WA ADAMU!

Katika kumbukumbu nne (4) za “INJILI” (Mathayo, Marko, Luka na Yohana), Bwana wetu Yesu Kristo amejitaja yeye Mwenyewe, takriban mara themanini (80), kama/kuwa “Mwana wa Adamu”. Cheo hiki kinatokana na kifungu katika unabii wa Danieli ambamo “mamlaka, na utukufu, na ufalme” vinatolewa kwa yule aliyetokea kama “Mwana wa Adamu” (Danieli 7:13-14). Mamlaka yake, kinasema kifungu hicho, “ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe”, na ufalme wake ni “ufalme usioweza kuangamizwa.”

Kama vile, neno “Mwana wa Mungu” linavyozungumza juu ya UUNGU WA BWANA WETU na neno “Mwana wa Daudi” linavyosisitiza juu ya cheo chake kama MFALME WA ISRAELI, vivyo hivyo neno “Mwana wa Adamu” linamtambulisha Yeye kama MWAKILISHI WA WANADAMU kwa ujumla.

Ni kama “Mwana wa Adamu” ndivyo ambavyo atatawala kama Mfalme wa ulimwengu, kama “Mfalme wa wafalme” kama tulivyoona hapo juu. Pia ni kama “Mwana wa Adamu” ndivyo ambavyo Yeye atayahukumu mataifa mara kabla tu ya ufalme Wake kusimikwa:

“Hapo atakapokuja MWANA WA ADAMU katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake; na mataifa yote watakusanyika mbele zake …” (Mathayo 25:31-32).

Kama “Mwana wa Adamu” pia atakuwa Mwamuzi katika hukumu ya mwisho kwenye Kiti cha Enzi, Kikubwa, Cheupe (Ufunuo 20:11-15).

“Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, bali amempa Mwana hukumu yote; Naye akampa amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni MWANA WA ADAMU” (Yohana 5:22,27).

Hakika, Mungu hangeweza kuwa mwenye haki zaidi katika mahusiano yake na wanadamu; Lakini jambo lililo bora zaidi ni kwamba, kama Mwana wa Adamu ndivyo ambavyo Bwana wetu, Yesu Kristo, alituwakilisha pale Kalvari, akilipa adhabu ya dhambi zetu ili apate kutukomboa kutoka katika hukumu ijayo…

“Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja…, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya WENGI” (Marko 10:45); Na katika “wakati ufaao”, Mtume Paulo aliinuliwa kutangaza habari njema kwamba Mpatanishi mkuu alikuwa amejitoa mwenyewe awe “fidia ya WOTE” (1 Timotheo 2:6).

Utukufu una Yeye KRISTO YESU Milele na Milele AMINA

Author: Festus Patta

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *